Mch. Dkt. Huruma Nkone
Mwenyekiti (Jeremiah Juma)-kushoto na Katibu (Joshua Shoo)
Dkt Huruma Nkone, mpenzi wa wasomi na watu wote wenye nia ya
kuwa wakuu katika Kristo Yesu na aliyeambatana na jeshi la vijana toka Victory
Christian Centre Tabernacle; Samwel Fred , Prosper Mwakitalima, Irene Lyatuu,
Eunice Kahogo na Bw. Gerson Fungo, baada ya kusoma “Zaburi 33:12” alianza kwa
kufafanua kwanini twahitaji kuombea mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya na
Taifa.
Aliyataja mambo kadhaa ya kuombea ikiwamo; 1.Kujiweka wakfu
kwa kutubu ili Bwana ayapokee maombi yetu. 2. Kuombea watu wote wanaotoa maoni;
kama walioandika Biblia walivuviwa wasiandike mawazo yao ila kile Mungu
alitaka, hata Babu wa kijijini anaweza kutoa mawazo mazuri yakulipeleka Taifa
katika njia sahihi. 3. Kuiombea Tume ya ukusanyaji maoni ya wananchi. 4.
Kuombea mchakato mzima usiingiliwe na dosari yeyote; wenye nia zao mbaya washindwe
na kusudi la Bwana litimie. n.k.
Ukumbi mzima ukamwomba Kristo Yesu ahusike |
Wito kwa wenye nia njema ni kuendelea kuombea mchakato huo ikiwa
ni pamoja kwenda kutoa maoni kupitia njia mbalimbali ambazo tume imetoa
kurahisisha ukusanyaji maoni ili Taifa hili lisiingie katika matatizo kwa matakwa
ya watu wachache. INAWEZEKANA NA BWANA YESU YU PAMOJA NASI.
Mratibu wa maombi (Abigael Nkindwa) akamwita akamsihi Bwana
Mama Mkubwa (Bernadetta Kasase)-kulia
na Mama Mdogo (Beatrice Isaya)-katikati wamezama;
Prosper Mwakitalima; Director wa CAMPUS MINISTRY, VCCT, naye aliitia jina la Mnazareth Yesu
Mwanasheria, Mtumishi wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Irene Lyatuu-kushoto, akamlingana Bwana
Namna hii lazima Bwana asikie kilio cha watumishi wake. Huyu ni Emmanuel Kashishila
Bw Gerson Fungo akashiriki kikamilifu
Bw Gerson Fungo akashiriki kikamilifu