Tuesday, January 22, 2013

UINJILISTI WA WANAFUNZI WA VYUO VIJIJINI (MISSION)


Huduma ya injili ni moja ya mabo wanayofanya wanafunzi waliiokoka mbali na masomo. Hufanya uinjilist kwa wanafunzi wenzao ambao hawajamjua Kristo na pia kwenda maeneo ya vijijini ambako injili haijafika kabisa au imefika kwa kiwangi kidogo.
Baadhi ya vyuo ambavyo vinatazamia kupeleka injili sawasawa na neno la Mungu katika Mathayo 28:19 (Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu).

Program ambazo hufanywa huko ni pamoja na;
Mkutano wa nje (crusade)
Uinjilist nyumba kwa nyumba (door to door) na mtu kwa mtu, wengine pia huwa na shamba kwa shamba
Ukarimu (charity) kama vile kugawa nguo, vifaa vya shule n.k
Mahubiri kwa njia ya Cinema pamoja na huduma zingine mbalimbali.

Baadhi ya vyuo vinavyotarajia kwenda kwa mwaka huu wa masomo ni pamoja na;

ARDHI--TAFES, 2-9, Feb wanaenda Mtwara kijiji cha Nanyamba. Idadi ya wanafunzi wanaotazamia kwenda ni zaidi ya 110.

                               Hawa ni wainjilisti watakaokuwa wakisimama madhabahuni kuongoza mashambulizi juu ya falme za giza, kuuteka ufalme ulioibiwa na mwovu ibilisi


ARDHI--CASFETA TAYOMI, 4-11, Feb, wanaenda Tanga- Kiomoni. Idadi ya watakaopeleka injili huko ni zaid ya wanafunzi 50.

Wana CASFETA ARDHI praise team wakiongoza wengine katika kusifu katika Roho na kweli

CASFETA Praise team wakihudumu kwenye mkutano wa nje katika moja ya mission


CASFETA  UDSM , Wataenda Chole Samvula, Pwani,  3-10 Februari.


Wengine wanaotazamia kwenda semister ijayo ni;

DIT- Kilimanjaro, July

UDSM-USCF-Rukwa, wanatarajia kwenda mwezi June

UDSM- MCF Morogoro-Ifakara, July

Sunday, December 30, 2012

KONGAMANO LA KIPEKEE KABISA LA KITAIFA LA CASFETA LAFANYIKA


Mchungaji Dkt Huruma Nkone, Mchungaji Kiongozi wa kanisa la Victory Christian Centre Tabernacle, pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya wanafunzi wa shule, vyuo na vyuo vikuu waliookoka  ya CASFETA. 

Akishilikiana na jopo la viongozi wake waliandaa kongamano la kipekee sana la viongozi na wanafunzi wote kama ilivyo kawaida kwa kila mwezi Desemba. Zilikuwa siku mbili zenye nguvu sana, tar 18 na 19 Desemba baada ya watu kuwasili kambini tar 17 pale zaidi ya wana-CASFETA 1000 walipokusanyika katika Shule ya St. Cornelius High School, Salasala, Tegeta, Dar-Es-Salaam. Walipata mafundisho, kufanyiwa maombezi na kuandaliwa kwa kazi kubwa ya kujenga chombo hicho, kanisa na Taifa kwa ujumla.

Kingine kikubwa ni kuwa, Mwaka huu 2012, CASFETA imesherehekea MIAKA 20 tangu kuanzishwa kwake (20th Anniversarry)

Ukumbi ukiwa umefurika; Maombezi yakiendelea 

Mkurugenzi Mkuu, Mch Dkt Huruma Nkone  

 Makamu Mkurugenzi Mkuu, Mch Weston Sambo

Katibu Mkuu, Bi Florence Mbago  

Kelvin Ngonyani; Mwenyekiti wa CASFETA wa Taifa wa wanafunzi(RAISI); Mwanafunzi wa SUA

Mch Dkt Huruma Nkone (Katikati), Bi. Florence Mbago(Kushoto) & Mch Weston Sambo(Kulia)

Maombi yanaendelea kufanyika. Kizazi kiletacho mabadiliko chaandaliwa

CASFETA ASSOCIATE, Ev Gregory Daudi (kushoto) akiwa na Mch Dkt Huruma Nkone 

Mkurugenzi wa CASFETA Kinondoni, Dkt Dickson Mkoka

Rose Mushi

Mch Julius Mkenda (katikati) na Mkewe (Bi Haika Mkenda) wakipokea toka kwa Mkurugenzi CASFETA


Katibu Mkuu, Bi Florence Mbago alikuja na mmewe, Bw Lucas Mbago (katikati)

Wana CASFETA wakiwa makini mafundisho yanapotolewa

Dar Praise & Worship Team wakaimba wimbo wa shukrani kwa Mungu kwa Miaka Ishirini ya CASFETA

John Lisu akaongoza sherehe za kumsifu Mungu kwa Miaka ishirini ya CASFETA

Baadhi ya wanafunzi wa vyuo wakiachilia baraka kwa wadogo zao ili wafike vyuo vikuu

Kila pando la Ibilisi lang'olewa, Bwana anapanda kitu ndani ya binti huyu; Hakika Taifa linaenda kupona

Kila pando la Ibilisi lang'olewa, Bwana anapanda kitu ndani ya binti huyu; Hakika Taifa linaenda kupona

Hawa ni sehemu ya  wanaCASFETA waliohudhuria kongamano

Wednesday, December 26, 2012

CHRISTMAS PRODUCTION YAFANA NDANI YA VCCT

Moja ya matamasha makubwa yanayochukua nafasi hapa jijini Dar, Christmas Production inaendelea kufana. Tukio hili hufanyika kila tar 26 Disemba 2012, siku moja baada ya siku Mwokozi wetu Yesu Kristo alipozaliwa. Ninapoandika,  tukio hili linaendelea na watu wanamsifu na kumwabudu Mungu kwa namna nisiyoweza elezea. Ndani ya nyumba wapo Rivers of Joy International, Glorious Celebration, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Amani Isayah, Bomby Johnson, Samuel Yonah, President Chavala, Mc Pilipili, CASFETA Dar P & W team.   


         Mch. Dkt Huruma Nkone, Mchungaji Kiongozi na mbeba maono 

                                                                       Mch Joyce Nkone
Ukumbi umefurika; watu wanamsifu aliyezaliwa 


 Upendo Nkone


 Upendo Kilahiro

MC...Samuel Sasali


Glorious Celebration; wametuabudisha na wao wanaabudu

 Upendo Nkone naye anaabudu


MC.. Pilipili na  Chris Mauki


Ada, aina ya Upendo Nkone mwingine anayejitokezea


Vijana chipukizi, ROJI  junior wa VCCT



Watumishi wa Mungu M Timothy Kyara na mkewe; UK & TANZANIA

Upendo Kilahiro & Mpelo Kapama, Kiongozi wa Muziki na Uimbaji, VCCT


Mc & President  Chavala


Bw Hillary Samwel (Kushoto) na Bw Misericodius (kushoto) wakimtukuza Mungu



Ukumbi haukutosha. Na watoto nao hawakubaki nyumbani; walikuwepo.

Naomi Venance; Binti aliyebarikiwa kiuimbaji. Toka UDSM, Mtoto wa VCCT.

Rivers Of Joy International; Wakiongoza umati mkubwa sana wa watu Kumsifu Mungu

Sunday, December 2, 2012

DKT HURUMA NKONE NA USCF MLIMANI WAOMBEA TAIFA NA MCHAKATO WA UANDISHI WA KATIBA MPYA KWA MZIGO SANA

Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, tar 01 Disemba, kuanzia saa 1 mpaka 3 usiku, Mch. Dkt. Huruma Nkone aliongoza maombi yenye nguvu ya kuombea mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya na Taifa kwa ujumla. Vijana na wanataaluma hao wa Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam chini Umoja wao uitwao University Students Christian Fellowship(USCF)-MLIMANI chini ya Jeremiah Juma (Mwenyekiti) na Joshua Shoo(Katibu), walipaza sauti zao na kuombea jambo hilo muhimu sana kwa mstakabari wa Taifa letu.

Mch. Dkt. Huruma Nkone 

Mwenyekiti (Jeremiah Juma)-kushoto na Katibu (Joshua Shoo)

Dkt Huruma Nkone, mpenzi wa wasomi na watu wote wenye nia ya kuwa wakuu katika Kristo Yesu na aliyeambatana na jeshi la vijana toka Victory Christian Centre Tabernacle; Samwel Fred , Prosper Mwakitalima, Irene Lyatuu, Eunice Kahogo na Bw. Gerson Fungo, baada ya kusoma “Zaburi 33:12” alianza kwa kufafanua kwanini twahitaji kuombea mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya na Taifa.


Aliyataja mambo kadhaa ya kuombea ikiwamo; 1.Kujiweka wakfu kwa kutubu ili Bwana ayapokee maombi yetu. 2. Kuombea watu wote wanaotoa maoni; kama walioandika Biblia walivuviwa wasiandike mawazo yao ila kile Mungu alitaka, hata Babu wa kijijini anaweza kutoa mawazo mazuri yakulipeleka Taifa katika njia sahihi. 3. Kuiombea Tume ya ukusanyaji maoni ya wananchi. 4. Kuombea mchakato mzima usiingiliwe na dosari yeyote; wenye nia zao mbaya washindwe na kusudi la Bwana litimie. n.k.  
Ukumbi mzima ukamwomba Kristo Yesu ahusike  
Wito kwa wenye nia njema ni kuendelea kuombea mchakato huo ikiwa ni pamoja kwenda kutoa maoni kupitia njia mbalimbali ambazo tume imetoa kurahisisha ukusanyaji maoni ili Taifa hili lisiingie katika matatizo kwa matakwa ya watu wachache. INAWEZEKANA NA BWANA YESU YU PAMOJA NASI.     

Mratibu wa  maombi (Abigael Nkindwa) akamwita akamsihi Bwana

Mama Mkubwa (Bernadetta Kasase)-kulia  na Mama Mdogo (Beatrice Isaya)-katikati wamezama;

Prosper Mwakitalima; Director wa CAMPUS MINISTRY, VCCT, naye aliitia jina la Mnazareth Yesu

Mwanasheria, Mtumishi wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Irene Lyatuu-kushoto, akamlingana Bwana

Eunice Kahogo-katikati; Coordinator CAMPUS MINISTRY,VCCT, aombea Katiba Mpya

Namna hii lazima Bwana asikie kilio cha watumishi wake. Huyu ni Emmanuel Kashishila


Bw Gerson Fungo akashiriki kikamilifu


Msomi mwingine akiomba Katiba mpya toka kwa Bwana na si wajanja wachache

Kila mtu kwa staili yake, bora tu Bwana apokee dua za watu wake kwa ajili ya Tanzania