Sunday, December 2, 2012

DKT HURUMA NKONE NA USCF MLIMANI WAOMBEA TAIFA NA MCHAKATO WA UANDISHI WA KATIBA MPYA KWA MZIGO SANA

Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, tar 01 Disemba, kuanzia saa 1 mpaka 3 usiku, Mch. Dkt. Huruma Nkone aliongoza maombi yenye nguvu ya kuombea mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya na Taifa kwa ujumla. Vijana na wanataaluma hao wa Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam chini Umoja wao uitwao University Students Christian Fellowship(USCF)-MLIMANI chini ya Jeremiah Juma (Mwenyekiti) na Joshua Shoo(Katibu), walipaza sauti zao na kuombea jambo hilo muhimu sana kwa mstakabari wa Taifa letu.

Mch. Dkt. Huruma Nkone 

Mwenyekiti (Jeremiah Juma)-kushoto na Katibu (Joshua Shoo)

Dkt Huruma Nkone, mpenzi wa wasomi na watu wote wenye nia ya kuwa wakuu katika Kristo Yesu na aliyeambatana na jeshi la vijana toka Victory Christian Centre Tabernacle; Samwel Fred , Prosper Mwakitalima, Irene Lyatuu, Eunice Kahogo na Bw. Gerson Fungo, baada ya kusoma “Zaburi 33:12” alianza kwa kufafanua kwanini twahitaji kuombea mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya na Taifa.


Aliyataja mambo kadhaa ya kuombea ikiwamo; 1.Kujiweka wakfu kwa kutubu ili Bwana ayapokee maombi yetu. 2. Kuombea watu wote wanaotoa maoni; kama walioandika Biblia walivuviwa wasiandike mawazo yao ila kile Mungu alitaka, hata Babu wa kijijini anaweza kutoa mawazo mazuri yakulipeleka Taifa katika njia sahihi. 3. Kuiombea Tume ya ukusanyaji maoni ya wananchi. 4. Kuombea mchakato mzima usiingiliwe na dosari yeyote; wenye nia zao mbaya washindwe na kusudi la Bwana litimie. n.k.  
Ukumbi mzima ukamwomba Kristo Yesu ahusike  
Wito kwa wenye nia njema ni kuendelea kuombea mchakato huo ikiwa ni pamoja kwenda kutoa maoni kupitia njia mbalimbali ambazo tume imetoa kurahisisha ukusanyaji maoni ili Taifa hili lisiingie katika matatizo kwa matakwa ya watu wachache. INAWEZEKANA NA BWANA YESU YU PAMOJA NASI.     

Mratibu wa  maombi (Abigael Nkindwa) akamwita akamsihi Bwana

Mama Mkubwa (Bernadetta Kasase)-kulia  na Mama Mdogo (Beatrice Isaya)-katikati wamezama;

Prosper Mwakitalima; Director wa CAMPUS MINISTRY, VCCT, naye aliitia jina la Mnazareth Yesu

Mwanasheria, Mtumishi wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Irene Lyatuu-kushoto, akamlingana Bwana

Eunice Kahogo-katikati; Coordinator CAMPUS MINISTRY,VCCT, aombea Katiba Mpya

Namna hii lazima Bwana asikie kilio cha watumishi wake. Huyu ni Emmanuel Kashishila


Bw Gerson Fungo akashiriki kikamilifu


Msomi mwingine akiomba Katiba mpya toka kwa Bwana na si wajanja wachache

Kila mtu kwa staili yake, bora tu Bwana apokee dua za watu wake kwa ajili ya Tanzania

Tuesday, November 20, 2012

Campus Night In Mbeya ni Next Next Level

Katika Weekend hii Big Events za wanafunzi zenye jina La Campus Night zimechukua mkondo wake katika mikoa ya Dodoma na Mbeya.

Blogger akiripoti kutoka Mbeya ameeleza kuwa Campus Night ya Mbeya imevunja Records ya Makusanyiko ya vijana na wanafunzi katika jiji hilo, event hiyo iliyokusanya wanafunzi zaidi ya 7000 ilikuwa na theme ya Raising The Standards.
Mwimbaji wa Injili anayevuma na ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Cha Uhasibu mkoani humo Ambwene Mwansongwe ndiye aliyeteka ukumbi kila aliposimama.
Wachekeshaji wanaovuma katika tasnia ya Gospel, King Chavalla na Mc Pilipili walinogesha Campus night yaJiji la Mbeya.
Wanenaji Wakuu Katika Usiku huo Dr. Huruma Nkone, Dr. Kimambo, Ms Rose Mushi na Mr. Msigwa wali Raise Standards za Wanafunzi.

Dr. Huruma Nkone aliyekuwa akifundusha Spiritual Transformation usiku huo alilipuka kinjilisti na kuwaambia wanafunzi 'Usharubalo na Utoz Toz,hautainua kiwango chako cha Kiroho, isipikuwa kwa kumpokea Yesu' akinukuu andiko la kutoka kwenye kitabu cha Yohana ikisema 'Mimi ndimi njia kweli na uzima, mtu haendi kwa Baba Isipokuwa kwa njia ya Mimi"
Dr. Kimambo alifundisha Academic and Career Challenges zinazowakabili wanafunzi.Dr. Kimambo ambaye ni Mwajiriwa wa Serikali yaUingereza nchini Tanzania alieleza 'changamoto za mfumo wa elimu na mahitaji ya soko la ajira ni tatizo linalo wakabili wanafunzi. Tatizo la Soft Skills mbali na ule ujuzi unaopatikana vyuoni ni changamoto pia.Mbali na changamoto hizo maendeleo na matumizi ya technolojia katika mfumo globalization ni changamoto inayowakabili wahitimu wa Elimu Ya Juu.
Mwanadada aliyekuwa msemaji pekee katika Campus night na mdogo wa umri kuliko wasemaji wote Dada Rose Mushi alifundisha RaisingThe Standard Of Ladies In the Campus. Rose Mushi ambaye ni Mchumi kwa taaluma na mwajiriwa wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Aliamsha hamasa kubwa ya vijana alipoanza kufundisha kutoka kwenye Kitabu Cha Mwanzo kwenye story ya Yusufu na Mke wa Potifa. Akifundisha Usiku huo Rose Mushi alisema ili kuinua Viwango vya Kiroho Vya Akina dada katika Campus inapaswa kwanza Ujue thamani yako kama Mdada, pili inakupasa kuachana na mambo yote ambayo yanakusababishia kukushikilia kwa mwanaume kama mi kufaulu, kama ni ada, kama ni laptop kama ambavyo Yusufu alimwachia vazi Mke wa Potifa.
Somo la Mahusiano lilifundishwa na Mr. Msigwa Meneja wa tawi la CRDB katika wilaya ya Mbozi. Alieleza uhusiano wowote wa mwanaume na mwanamke hauwezi kuwa mzuri kama wahusika wana uhusiano mbaya na Mungu wao.
Praise and Worship Leaders. Mr and Mrs Matthew Sasali

Event hiyo ilisimamiwa na Dr. Nyanda pamoja na Ze Blogger. Praise Team ilisimamiwa na Pastor Matthew Sasali na Rebecca Sasali
Dr. Nyanda, Rose Mushi na Papaa Ze Blogger hapo ilikuwa saa 1 Asubuhi baada ya event.

Matukio Katika Picha.
 Sehemu Ya Umati Wa watu
 Mrs. Rebecca Sasali akiongoza Praise Team
 Wanafunzi Waliotoka Mbele Kumpa Yesu Maisha Yao Zaidi ya wanafuzi 90 walimpa Yesu Maisha yao.
 Ndani Ya Uwepo
 Watu Wakienda Sawa ndani ya Ukumbi
 Full Shangwe Wanafunzi Wa Mbeya
 Chezea Nyomi
 Respected Event Manager Papaa Ze Blogger ndani ya Ukumbi
 Ukumbi Mzima Kidole namba tatuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 Watu Wakimpa Yesu Maisha Yao.
 Rose Moshi Kikazi zaidi
 Chezea Urefu
 Wakienda sawa
 Huu Mwili Khaaaa
 Pilipili Kikazi Zaidi ndani ya Mbeya
 Kikazi Zaidi hapa
 Safari Hii akaja na Style ya Sketi aiseeee ilikuwa nouma inaitwa "Usiombe Kusutwa'
 Dr. Maboko akizungumza kwenye Campus Night
 King Chavallaaaaaaaa akienda sawa ndani ya Campus Night
Jamaa kumbe akivua Kofia ni handsome sanaaaaaaaa

Wednesday, November 14, 2012

Home, Sweet Home! [Devotional]

Dear beloved students wherever you are, greetings in the might name of our Lord Jesus Christ!

I have this devotional for you today: Home, Sweet Home!

1 Thes.2:1-12

I suppose I had many reasons for taking the train home from college so many holidays. I did bring back bags of books and clothes, like most college guys. But the real reason was that nothing felt quite like home. Nothing was quite as comfortable as Mom cooking in the tiny kitchen, etc.

Home was warm, comfortable, a place where I was welcomed and loved even if I was a college man now, and out on my own. Home had a climate all its own.

Paul understood this as well as anyone. He knew that home is the one really effective climate for evangelism and for spiritual growth. So Paul not only brought others the Gospel in word, he created a sense of family by the way he loved every member of the Thessalonian church.

What people need today, perhaps even more than in other times, is that climate of warmth, intimacy, and caring that marks a loving home. The church (fellowship) that provides this climate will be sure to grow. And its members will become mature.

Personal Application


Build your church (fellowship) as birds build nests—one tiny twig of love at a time.

Quotable: We Exist To Provide Love And Care For One Another...

through sharing each other's needs, burdens, and joys through serving each other in a sacrificial way through learning how to love and be loved.

God in His grace, has given us to each other. An integral part of our life as His body is caring for and supporting each other.—From the Mission Statement, Crossroads Community Church.
Yours,
Dr. Huruma Nkone

VCCT Campus Ministry ndani Ya Mabibo Fellowship "Qualities Of a Christian Graduate"

Fellowship Ya Wanafunzi Wa Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam Wanaoishi Kwenye Campus Ya Mabibo chini ya Fellowship ya MCF siku ya Jana Waliandaa Maalum Kwa ajili ya Semina Ya Kujifunza Tabia/Miyenendo/Sifa za Muhitimu Aliyeokoka apart from "Certificates" Ya Chuo.

Samuel Sasali mmoja wa wadau wa Campus Ministry alifafanua kwa Kina Tabia kadha Wa Kadha Zilizo Chini ya Mwamvuli wa 1. Integrity 2. Commitment 3. Trustworthy 4. Analytic 5. Transparent 6.Sociability etc. Na Mwisho Mwenyekiti wa Fellowship akaongoza Maombi Kwa ajili ya Kutengeneza Mkakati Wa Kuandaa Wakristo Kuchukua nafasi katika maeneo yote yenye Ushawishi Katika Taifa la Tanzania.



Prayer Time Ndani Ya MCF Mabibo...



Mwenyekiti Akiomba na Keyboardist



Twende Sawa



Prayer Time



Watu wakiliitia Jina la Bwana.



Sasa jeee



Chezea Wewe Uchovu wa Kazini Jumlisha na wakufundisha



Khaa Wanakaa Kijinsia sana hawa Fellowship

Tuesday, November 13, 2012

Campus Night In Singida


Wanafunzi Wa Mkoa Wa Dar-es-Salaam Chini Ya Tafes Waadhimisha Wiki la Uinjilisti Pamoja

Wanafunzi wa Elimu Ya Juu Katika Vyuo Mbalimbali Katika Mkoa wa Dar-es-Salaam walio chini ya affiliation ya TAFES wamehitimisha wiki la Uinjilisti kwa kufanya Ibada Maalum katika Kanisa la DPC lililo Dar-es-Salaam.
Katika Ibada hiyo iliyoanza majira ya saa 8 Mchana na Kuhudhuriwa na Wanafunzi, Tafes Staff, Associates na Watumishi wengine ilikuwa ya aina yake siku ya jana. Pastor Safari pamoja na Rivers Of Life ndio walioongoza Praise and Worship kwa siku ya Jana.

Pastor Carlos kama ilivyo ada ya Karama yake ya Ualimu alifundisha namna ya kuwafikia wengine kupitia kubadilishwa kwako kupitia neno. Akifundisha katika Jioni ya Jana Pastor Carlos alisema "You cant live a life of impact, without being impacted kwanza, huwezi kuwafikia wengine kabla wewe mwenyewe hujafikiwa kwanza, ni lazima neno liwe limefanya jambo kwenye maisha yako ndipo utakapoweza kutenda jambo kwa wengine"Tafes ni Organization inayofanya Kazi na wanafunzi wa Vyuo Vya Elimu ya Juu hapa Tanzania kwa Kuwafikia kwa neno la Mungu na Kuwafundisha kwa ajili ya maisha ya Utauwa na Ucha Mungu. Tafes haipo chini ya dhehebu fulani ni Interdenominational Organisation.

Pia katika Siku ya Jana alikuwepo Director wa Tafes Tanzania, Mr. Rex, Alikuwepo Makamu Mwenyekiti wa Board Mr. Ben na Pia alikuwepo Mwenyekiti wa Tafes Mkoa wa Dar-es-Salaam Mr. Simalenga.



 Inter Collage Praise Team Ikihudumu siku ya Jana Ndani ya DPC




 Twende Kazi




 Kulia Viongozi wa Taifa na Mkoa wakiwa kwenye Ibada




 Wanafunzi ndani ya DPC




 Pastor Carlos akishusha nondo




 Twende Kazi Jembe




 Amepona kabisa Mguu kwa sasa




 Ze Blogger Ndani ya Tafes