Monday, November 4, 2013

SPECIAL CAMPUS SERVICE (GET FULLY CHARGED) IMEKUWA YA AINA YAKE

Ile baada maalum ya kuweka wakfu wanafunzi wa vyuo vikuu kwa ajili ya mwaka mpya wa masomo ambayo iliandaliwa na Kanisa la Victory Christian Centre Tabernacle (VCCT) linaloongozwa na Mch. Dr. Huruma Nkone chini ya Idara ya Wanafunzi (Campus Ministry) imekuwa ya aina yake na ya kipekee. wanafunzi toka kila kona ya jiji la Dar es salaam walikusanyika katika kanisa la VCCT lililopo Mbezi A jijini Dar es salaam

Kwaya na vikundi mbali mbali vilikuwepo kumtukuza Mungu katika siku hii. miongoni mwa vikundi vilivyo hudumu ni Mabibo Christian Fellowship Choir toka UDMCF, Kwaya ya CASFETA Dar es salaam, Kwaya toka Chuo cha DIT, Kwaya toka Ardhi University (TAFES Praise team) na Kundi la Glorious Worship Team (GWT) bila kusahau watoto wa nyumba ya VCCT The Rivers of Joy International (RoJI).

Ibada hii ya shangwe iliongozwa na Dr. Huruma Nkone na kuratibiwa na Idara ya wanafunzi (Campus Ministry).

Katika siku hii wanafunzi wa vyuo walipata fursa ya kusikiliza neno toka kwa Mch. Dr. Nkone, na baada ya hapo, Dr. Nkone alifanya maombi maalum kwa ajili ya wanafunzi kwa ajili ya kuwaweka wakfu kwa ajili ya mwaka mpya wa masomo, na baada ya ibada Dr. Nkone alikutana na wanafunzi hao kwenye eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili yao na kupata soda pamoja na wanafunzi hao na kisha kuomba baaraka kwa ajili yao.

Tukio la kupiga picha lilifuata ambapo viongozi wa fellowship walipata fursa ya kupiga picha na Mchungaji Dr. Nkone katika red carpet iliyoandaliwa kwa ajili yao.

Angalia matukio yalivyokwenda 


watu waliohudhuria

DR. Nkone akishusha nondo

wanafunzi wakiwekwa wakfu

watu wakimpa Yesu maisha yao

Take note.....



Dr. Nkone akiongea na wanafunzi kwa karibu zaidi

The Red Carpet..


Moderator 1st service, CEO wa MANCON EA LTD, Brother Pro


DIT Choir wakimtuza MUngu
watu wakienda sawa
The Bomby, Fredy Msungu na Amani Kapama wakifanya kweli
Ardhi University Tafes Praise team
Campus Ministry team na Dr. Nkone
Kairuki University Pamoja na Mch DR. Nkone
Pokeaaaa kwa Jina la Yesu Kristo

UDMCF Praise team wakiimba


RoJI watoto wa Nyumbani wakiimba








































More Pictures to Come.............

Tuesday, January 22, 2013

UINJILISTI WA WANAFUNZI WA VYUO VIJIJINI (MISSION)


Huduma ya injili ni moja ya mabo wanayofanya wanafunzi waliiokoka mbali na masomo. Hufanya uinjilist kwa wanafunzi wenzao ambao hawajamjua Kristo na pia kwenda maeneo ya vijijini ambako injili haijafika kabisa au imefika kwa kiwangi kidogo.
Baadhi ya vyuo ambavyo vinatazamia kupeleka injili sawasawa na neno la Mungu katika Mathayo 28:19 (Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu).

Program ambazo hufanywa huko ni pamoja na;
Mkutano wa nje (crusade)
Uinjilist nyumba kwa nyumba (door to door) na mtu kwa mtu, wengine pia huwa na shamba kwa shamba
Ukarimu (charity) kama vile kugawa nguo, vifaa vya shule n.k
Mahubiri kwa njia ya Cinema pamoja na huduma zingine mbalimbali.

Baadhi ya vyuo vinavyotarajia kwenda kwa mwaka huu wa masomo ni pamoja na;

ARDHI--TAFES, 2-9, Feb wanaenda Mtwara kijiji cha Nanyamba. Idadi ya wanafunzi wanaotazamia kwenda ni zaidi ya 110.

                               Hawa ni wainjilisti watakaokuwa wakisimama madhabahuni kuongoza mashambulizi juu ya falme za giza, kuuteka ufalme ulioibiwa na mwovu ibilisi


ARDHI--CASFETA TAYOMI, 4-11, Feb, wanaenda Tanga- Kiomoni. Idadi ya watakaopeleka injili huko ni zaid ya wanafunzi 50.

Wana CASFETA ARDHI praise team wakiongoza wengine katika kusifu katika Roho na kweli

CASFETA Praise team wakihudumu kwenye mkutano wa nje katika moja ya mission


CASFETA  UDSM , Wataenda Chole Samvula, Pwani,  3-10 Februari.


Wengine wanaotazamia kwenda semister ijayo ni;

DIT- Kilimanjaro, July

UDSM-USCF-Rukwa, wanatarajia kwenda mwezi June

UDSM- MCF Morogoro-Ifakara, July